Job Yustino Ndugai
From Wikipedia, the free encyclopedia
Remove ads
Job Yustino Ndugai (21 Januari 1960 – 6 Agosti 2025) alikuwa mbunge wa jimbo la Kongwa katika Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.[1] Alikuwa mwanachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Maisha na kazi
Job Ndugai alihudumu kama mbunge wa jimbo la Kongwa kuanzia mwaka 2000 hadi kifo chake mwaka 2025. Tangu tarehe 17 Novemba 2015 hadi 6 Januari 2022 alikuwa Spika wa Bunge la Tanzania. Kabla ya hapo, alikuwa Naibu Spika wa Bunge hilo kuanzia mwaka 2010.
Mnamo Januari 2022, alijiuzulu wadhifa wake wa uspika baada ya kutokea mvutano wa kisiasa na rais Samia Suluhu Hassan.[2]
Elimu
Job Ndugai alipata elimu yake ya sekondari katika shule ya Sekondari ya Kibaha na baadaye kujiunga na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, ambako alisomea sayansi ya wanyama. Pia alisomea masuala ya bunge katika vyuo vya kimataifa ikiwa ni pamoja na India na Ujerumani.
Tazama pia
Marejeo
Wikiwand - on
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.
Remove ads