Job Yustino Ndugai

From Wikipedia, the free encyclopedia

Job Yustino Ndugai
Remove ads

Job Yustino Ndugai (21 Januari 19606 Agosti 2025) alikuwa mbunge wa jimbo la Kongwa katika Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.[1] Alikuwa mwanachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Thumb
Job Ndugai, 2017

Maisha na kazi

Job Ndugai alihudumu kama mbunge wa jimbo la Kongwa kuanzia mwaka 2000 hadi kifo chake mwaka 2025. Tangu tarehe 17 Novemba 2015 hadi 6 Januari 2022 alikuwa Spika wa Bunge la Tanzania. Kabla ya hapo, alikuwa Naibu Spika wa Bunge hilo kuanzia mwaka 2010.

Mnamo Januari 2022, alijiuzulu wadhifa wake wa uspika baada ya kutokea mvutano wa kisiasa na rais Samia Suluhu Hassan.[2]

Elimu

Job Ndugai alipata elimu yake ya sekondari katika shule ya Sekondari ya Kibaha na baadaye kujiunga na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, ambako alisomea sayansi ya wanyama. Pia alisomea masuala ya bunge katika vyuo vya kimataifa ikiwa ni pamoja na India na Ujerumani.

Tazama pia

Marejeo

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads