Rais

From Wikipedia, the free encyclopedia

Rais
Remove ads

Rais (kutoka Kiarabu: رئیس) ni cheo cha mkuu wa nchi katika serikali ya jamhuri, na pengine mkuu wa taasisi fulani ("mwenyekiti"). Katika baadhi ya mifumo, rais pia huwa mkuu wa serikali. Majukumu yake hutofautiana kulingana na katiba ya nchi husika, yakiwemo uongozi wa serikali, uwakilishi wa taifa kimataifa, na utekelezaji wa sheria. Pia, neno "rais" hutumika kumaanisha mkuu au mwenyekiti wa taasisi, shirika, au chombo kingine rasmi.

Thumb
Rais wa Tanzania, John Magufuli (Kulia) akiwa na Dr. Salem Al Ismaily wa Oman

Rais wa nchi huwa anachaguliwa ama na wananchi wote au na bunge. Katika nchi kadhaa kuna pia mkutano maalumu unaoitishwa kwa uchaguzi wa rais pekee, kama vile Marekani[1] au Ujerumani [2].

Kuna aina mbili za rais kufuatana na katiba za nchi mbalimbali:

Katika muundo wa serikali ya kibunge shughuli za serikali zinasimamiwa na waziri mkuu. Madaraka ya rais katika muundo huo hufanana na madaraka ya mfalme wa kikatiba isipokuwa hayupo kama rais kwa muda wa maisha yake kama mfalme.

Katika nchi chache, yaani Uswisi, San Marino na Uruguay, kazi za rais hazitekelezwi na mtu mmoja bali na kamati ya viongozi kwa ujumla, kama Halmashauri ya Shirikisho ya Uswisi.

Remove ads

Marejeo

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads