Julie Billiart

From Wikipedia, the free encyclopedia

Julie Billiart
Remove ads

Julie Billiart (Cuvilly, Ufaransa, 12 Julai 1751Namur, Ubelgiji, 8 Aprili 1816) alikuwa bikira aliyeanzisha kwa ajili ya malezi ya wasichana shirika la Masista wa Bibi Yetu wa Namur mwaka 1803[1].

Thumb
Mt. Julie Billiart alivyochorwa mwaka 1830.

Alikuwa maarufu kwa upendo wake wa pekee akaeneza kwa bidii ibada kwa Moyo Mtakatifu wa Yesu[2].

Siku hizi masista wake ni 2,000 hivi, nao wanaishi katika nchi 20 za mabara matano, zikiwemo Kenya na Tanzania.

Alitangazwa mwenye heri na Papa Pius X tarehe 13 Mei 1906 halafu mtakatifu na Papa Paulo VI tarehe 22 Juni 1969.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe ya kifo chake[3].

Remove ads

Tazama pia

Tanbihi

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads