Kaaba

From Wikipedia, the free encyclopedia

Kaaba
Remove ads

Kaaba ni jengo lenye umbo la mchemraba lililopo ndani ya msikiti mkuu wa Masjid al-Haram mjini Makka nchini Saudia.

Thumb
Kaaba ikizungukwa na waumini.

Inatazamwa kama mahali patakatifu katika imani ya Uislamu. Waislamu huamini ni nyumba ya Mungu iliyojengwa kiasili na Adamu na baadaye na Abrahamu.

Ni lengo la safari ya hija. Kila Mwislamu mwenye uwezo anatakiwa kuitembelea angalau mara moja katika maisha yake.

Waislamu wanatakiwa kuielekea Kaaba wakati wa kusali na kila msikiti huwa na sehemu ya mihrabu inayotazama Makka. Mwelekeo huu huitwa kibla.

Remove ads

Viungo vya nje

WikiMedia Commons
WikiMedia Commons
Wikimedia Commons ina media kuhusu:
Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads