Kireno
From Wikipedia, the free encyclopedia
Kireno (Português - tamka "purtuGESH") ni lugha ya Kirumi inayozungumzwa hasa nchini Ureno na Brazil, lakini pia Kusini mwa Afrika, Asia Kusini na Asia Kusini-Mashariki.
"Pt" inaelekezwa hapa. Kwa matumizi mengine, tazama Pt (maana).
Kireno Português (pt) |
|
---|---|
Lugha | |
Asili | Ureno Brazili Angola Msumbiji Guinea-Bissau Timor ya Mashariki Cabo Verde São Tomé na Príncipe |
Wasemaji |
L1 : 230 Milioni |
Familia za lugha | Kihindi-Kiulaya Kiitalia Kilatini Kirumi Kirumi Magharibi Kirumi Kusini Kireno-Galicia |
Aina za Awali | Kilatini cha Kale Kilatini halisin Kireno-Galicia |
Mfumo wa kuandika | Kilatini |
Lugha Rasmi | |
Lugha rasmi kwa | Ureno Brazili Angola Msumbiji Guinea-Bissau Timor ya Mashariki Cabo Verde São Tomé na Príncipe |
Nambari za Msimbo | |
ISO 639-1 | pt |
ISO 639-2 | por |
Glottolog | port1283 |
![]() Wasemaji wa Kireno duniani |
Imekuwa lugha ya kimataifa kutokana na historia ya ukoloni ya Ureno ikiwa na wasemaji wa lugha ya kwanza milioni 210-215; pamoja na wasemaji wa lugha ya pili kuna watu milioni 270 duniani wanaoelewana kwa Kireno, hivyo ni lugha ya 5 au ya 6 ulimwenguni.
Kutokana na historia ya ukoloni Kireno kimepatikana katika nchi zifuatazo:
Kireno kama lugha rasmi
Lugha ya kieneo
Historia ya lugha
Kireno ni moja kati ya lugha za Kirumi maana yake kimetokana na Kilatini cha Dola la Roma lililotawala eneo la Ureno kwa karne nyingi.
Ni karibu hasa na Kigalicia kinachozungumzwa katika Hispania ya Kaskazini.
Wareno waliacha lugha yao katika makoloni yao. Leo hii idadi ya wasemaji katika Ureno ni milioni 10 tu - idadi kubwa kabisa wako nje ya Ureno, hasa Brazil.
Kireno kilisambaa zaidi katika karne ya 20 kwa sababu Wareno waliondoka Ureno kutafuta kazi katika nchi nyingi za Ulaya. Vilevile kuna Wabrazil na Waangola waliotoka kwao kuhamia penginepo wakienda na lugha yao.
Viungo vya nje
- makala za OLAC kuhusu Kireno Ilihifadhiwa 4 Agosti 2021 kwenye Wayback Machine.
- lugha ya Kireno katika Glottolog
- http://www.ethnologue.com/language/por
![]() |
Makala hii kuhusu mambo ya lugha bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Kireno kama historia yake, uenezi au maendeleo yake? Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |
Wikiwand - on
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.