Kitabu cha Baruku

From Wikipedia, the free encyclopedia

Remove ads

Kitabu cha Baruku ni kimojawapo kati ya vitabu vya deuterokanoni vya Agano la Kale katika Biblia ya Kikristo.

Uandishi

Kadiri ya utangulizi wake (Bar 1:1-14), kiliandikwa na Baruku, karani wa nabii Yeremia, wakati wa uhamisho wa Wayahudi huko Babuloni katika karne ya 6 K.K..

Hata hivyo wataalamu wanaona kiliandikwa katika karne ya 2 K.K. moja kwa moja katika lugha ya Kigiriki, isipokuwa labda sehemu ya pili inatokana na andiko asili la Kiebrania.

Mazingira

Kitabu kinatuingiza katika Uyahudi wa mtawanyiko na kutuonyesha jinsi maisha maadilifu ya kidini yalivyodumishwa kwa kuhusiana na Yerusalemu, kwa kudumisha sala na kushika Torati.

Ufafanuzi

Kama vitabu vyote vya Biblia, hiki pia kinatakiwa kisomwe katika mfululizo wa historia ya wokovu ili kukielewa kadiri ya maendeleo ya ufunuo wa Mungu kwa binadamu.

Viungo vya nje

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads