Kitabu cha Hagai
From Wikipedia, the free encyclopedia
Remove ads
Kitabu cha Hagai ni kimojawapo kati ya vitabu 12 vya Manabii wadogo ambavyo, pamoja na vingine vingi, vinaunda Tanakh, yaani Biblia ya Kiebrania. Hivyo ni pia sehemu ya Agano la Kale katika Biblia ya Kikristo.
Kama vitabu vingine vyote vya Biblia, hiki pia kinatakiwa kisomwe katika mfululizo wa historia ya wokovu ili kukielewa kadiri ya maendeleo ya ufunuo wa Mungu kwa binadamu.
Mwandishi na muda
Kazi ya nabii huyo kati ya Agosti na Desemba ya mwaka 520 KK, wakati uleule alipoanza nabii Zekaria, ni mwanzo wa kipindi cha mwisho cha unabii katika Israeli kabla ya ujio wa Yohane Mbatizaji na Yesu Kristo.
Mazingira
Kabla ya uhamisho wa Babeli, ujumbe wa manabii ulitishia mara nyingi adhabu ya Mungu kwa uasi wa taifa lake.
Wakati wa uhamisho ujumbe ulikuwa wa faraja zaidi.
Ule wa Hagai na Zekaria ulilenga ustawi wa Wayahudi waliokuwa wamerudi Yerusalemu mwaka 538 K.K. ili kujenga upya hekalu, lakini walichelewa kutekeleza azma yao, kutokana na upinzani na mahangaiko ya kujipatia riziki katika mazingira magumu.
Mbaya zaidi, walikaribia kukata tamaa. Kwa changamoto ya manabii wao, gavana Zerubabeli na kuhani mkuu Yoshua waliongoza wananchi kukazania ujenzi huo na kuukamilisha mwaka 515 KK.
Remove ads
Muhtasari
Wikiwand - on
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.
Remove ads