Makemake

From Wikipedia, the free encyclopedia

Makemake
Remove ads

Makemake (alama: 🝼;[1] tamka kama ni Kiswahili; jina rasmi: 136472 Makemake) ni sayari kibete inayozunguka jua letu katika umbali mkubwa kwenye ukanda wa Kuiper.

Thumb
Makemake na mwezi wake.

Iligunduliwa na wanaastronomia Michael E. Brown, Chad Trujillo na David Rabinowitz kwenye paoneaanga pa Mount Palomar tarehe 31 Machi 2005.

Jina

Jina lilichaguliwa kutokana na mungu muumbaji aliyeitwa "Makemake" katika dini asilia ya Kisiwa cha Pasaka (Easter Island, kwenye Bahari ya Pasifiki). Kuna mapatano katika Umoja wa Kimataifa wa Astronomia kutumia majina ya miungu ya dini mbalimbali kwa magimba yanayoendelea kugunduliwa katika ukanda wa Kuiper. Asili ya jina iko katika lugha ya Kipolinesia na katika dini yao ni muumbaji wa binadamu na mungu wa rutuba. Makemake aliabudiwa kwa umbo la ndege wa bahari. Ishara yake ilikuwa mwanamume mwenye kichwa cha ndege.[2]

Remove ads

Muundo na tabia

Hakuna habari nyingi za uhakika kutokana na umbali wa gimba hili na kwa sababu hadi sasa hakuna chombo cha angani kilichopita karibu nayo. Lakini Makemake inaonekana ni hasa mwamba na barafu ilhali katika baridi iliyopo mbali na jua barafu huwa ngumu kama mwamba.

Marejeo

Viungo vya Nje

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads