Metodi wa Olimpo

From Wikipedia, the free encyclopedia

Metodi wa Olimpo
Remove ads

Metodi wa Olimpo (alifariki mwaka 311 hivi) alikuwa askofu wa Olimpo (Lycia) na mfiadini kutoka Anatolia (leo nchini Uturuki)[1].

Thumb
Kifodini chake.

Taarifa za kwanza juu yake ziliandikwa na mtakatifu Jeromu[2]

Tangu kale anaheshimiwa na Wakatoliki na Waorthodoksi kama mtakatifu na babu wa Kanisa.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 20 Juni[3]

Maandishi

Metodi aliandika sana na kwa ufasaha kuhusu masuala ya teolojia, akipinga uzushi wa wakati wake na hasa ule wa mafundisho kadhaa ya Origen.

Kwa bahati mbaya, vitabu vyake vimepotea kwa kiasi kikubwa. Kilichotufikia kizima kwa Kigiriki kinahusu ubikira (Symposion e peri hagneias).[4]

Kati ya matoleo ya maandishi yake kuna: Patrologia Graeca, XVIII; Jahn, S. Methodii opera et S. Methodius platonizans (Halle, 1865); Bonwetsch, Methodius von Olympus: I, Schriften (Leipzig, 1891).

Remove ads

Tazama pia

Tanbihi

Marejeo mengine

Viungo vya nje

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads