Mkoa wa Unguja Mjini Magharibi
From Wikipedia, the free encyclopedia
Remove ads


Mkoa wa Unguja Mjini Magharibi ni kati ya mikoa 31 ya Tanzania. Uko Unguja ambacho ni kisiwa kikubwa cha Jamhuri ya Watu wa Zanzibar. Unapakana na mikoa yote miwili mingine ya kisiwa hicho: Mkoa wa Unguja Kusini na Mkoa wa Unguja Kaskazini mbali ya Bahari Hindi. Eneo la mkoa ni km² 230 ambako kuna jumla ya wakazi 893,169 kadiri ya sensa ya mwaka 2022 [1]. Walikuwa 593,678; Mjini 223,033 na Magharibi 370,645 katikasensa ya mwaka 2012[2]. Makao makuu ya mkoa yako Zanzibar. Sehemu ya jiji hilo, maarufu kama Mji Mkongwe, imeorodheshwa na UNESCO kama Urithi wa Dunia.
Msimbo wa posta ni namba 71000.
Mkoa huu una wilaya tatu ambazo ndizo Mjini, yaani Jiji la Zanzibar, Unguja Magharibi A na Unguja Magharibi B.
Remove ads
Marejeo
Tazama pia
Viungo vya nje
Wikiwand - on
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.
Remove ads