Mumbi

Ndege wakubwa wa familia Bucorvidae From Wikipedia, the free encyclopedia

Mumbi
Remove ads

Mumbi, hondo-ardhi au mbizi wa nyika ni ndege wa jenasi Bucorvus, jenasi pekee ya familia Bucorvidae. Wana mnasaba na hondohondo na hadi juzi waliainishwa katika familia Bucerotidae, lakini ndege hawa ni wakubwa sana na hukaa ardhini takriban saa zote. Urefu wao unaweza kufika mita moja na upana wa mabawa mita mbili. Mumbi ni weusi isipokuwa manyoya makuu meupe ya mabawa. Wana ngozi tupu pande zote za macho na koo yao yenye rangi nyekundu na/au buluu.

Maelezo zaidi Uainishaji wa kisayansi, Ngazi za chini ...

Spishi zote mbili zinatokea Afrika chini ya Sahara. Hula wadudu wakubwa, makoa, nyungunyungu, mijusi, nyoka na hata kuchakulo na sungura. Jike huyataga mayai 1-3 katika tundu asilia ya mwamba au mti. Hafungwi ndani ya tundu tofauti na spishi za hondohondo. Hata yakiwapo mayai 2 au 3, kinda mmoja tu aishi. Ndugu wa jozi inayozaa husaidia kuwaletea jike na kinda chakula.

Remove ads

Spishi

Spishi ya kabla ya historia

  • Bucorvus brailloni (Miocene ya Maroko)

Picha

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads