Duara

From Wikipedia, the free encyclopedia

Duara
Remove ads
Remove ads

Duara ni umbo la mviringo bapa yaani katika ubapa linalofanana na herufi "o".

Thumb
Duara na nusukipenyo (rediasi)

Katika jiometria duara huelezwa kuwa mchirizo uliofungwa na umbali wa kila nukta ya mchirizo ni sawa kutoka kitovu cha duara.

Mstari wa nje wa duara huitwa mzingo. Katikati yake ni kitovu. Mstari usioonyoka kutoka kitovu hadi mzingo huitwa rediasi au nusukipenyo. Mstari wowote kutoka upande mmoja wa mzingo hadi upande mwingine unaopita kwenye kitovu huitwa kipenyo.

Kiwango cha kipenyo (d) ni mara mbili kiwango cha nusukipenyo (r).

Katika mahesabu ya duara namba inayoandikwa kwa herufi ya kigiriki π (tamka: pi) ni muhimu. Ni sawa na urefu wa mzingo (c) uliogawiwa kwa urefu wa kipenyo na ni takriban 3.14159.

Eneo la duara (a) ni sawa na zao ya nusukipenyo (r) mara nusukipenyo halafu mara π (a ni π mara (r mara r)).

Remove ads

Viungo vya nje

WikiMedia Commons
WikiMedia Commons
Wikimedia Commons ina media kuhusu:

Marejeo

Loading content...
Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads