Mwana wa Adamu
From Wikipedia, the free encyclopedia
Remove ads
Mwana wa Adamu (kwa Kiebrania בן–אדם, ben-'adam, yaani binadamu; kwa Kigiriki "ὁ υἱὸς τοὺ ἀνθρώπου", ho huios tou anthropou, "mwana wa mtu") ni jina lililotumiwa na Yesu Kristo katika kujitaja ili kujitambulisha. Limeandikwa mara nyingi katika Injili, Matendo ya Mitume na Kitabu cha Ufunuo, ingawa halikuendelea kutumiwa sana na Wakristo waliopendelea jina "Mwana wa Mungu".[1][2][3]
Mara 81 linapatikana katika Injili, lakini daima mdomoni mwa Yesu.[4] Inawezekana mwenyewe alilipenda kwa sababu Wayahudi walikuwa hawalitumii kwa kulipotosha kama ilivyokuwa kwa jina Masiya walilolielewa kisiasa.
Pia jina hilo liliweza kudokeza unyonge wa kibinadamu ambao Mwana aliutwaa, pamoja na utukufu wake ujao, kadiri ya kitabu cha Danieli (7:13-14).
Remove ads
Tanbihi
Marejeo
Wikiwand - on
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.
Remove ads