Utukufu

From Wikipedia, the free encyclopedia

Utukufu
Remove ads

Utukufu (kwa Kiebrania הוד, hod, na כבד, kabod, "uzito"; kwa Kigiriki δόξα, doxa, "tathmini"; kwa Kiingereza glory kutoka Kilatini gloria, "umaarufu") ni hasa sifa ya Mungu anapojitokeza kwa viumbe.

Thumb
Mozaiki ya Kugeuka sura, Monasteri ya Mt. Katerina, Mlima Sinai, Misri.

Katika Biblia na Ukristo utukufu ni muhimu sana, kwa sababu unatazamwa kuwa ndio lengo la uumbaji[1] ili kwa njia hiyo watu waokoke.[2]

Katika Kut 33:20, Musa aliambiwa mtu yeyote hawezi kuona utukufu huo na kuendelea kuishi.

Yesu aliwafundisha wafuasi wake kutenda mema, ili watu wakiona wamtukuze Baba wa mbinguni (Math 5:16).

Kadiri ya Injili Ndugu, Yesu alionekana na wanafunzi watatu akiwa katika utukufu pamoja na Musa na Elia (Lk 9:29-32).

Utukufu utashirikishwa kwa binadamu waadilifu watakapofufuliwa siku ya mwisho

Kinyume cha kulenga utukufu huo kutoka kwa Mungu, mara nyingi watu wanajitafutia sifa kutoka kwa wenzao (Yoh 12:43). Ndiyo dhambi ya majivuno inayozuia imani.[3]

Remove ads

Tanbihi

Viungo vya nje

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads