Nabii Yoeli

From Wikipedia, the free encyclopedia

Nabii Yoeli
Remove ads

Nabii Yoeli (kwa Kiebrania יואל, Yoel, maana yake YHWH ni Mungu) alikuwa nabii wa Israeli ya Kale, labda katikati ya karne ya 4 KK.

Thumb
Nabii Yoeli alivyochorwa na Michelangelo katika kuta za Cappella Sistina, Vatikano.

Ujumbe wake unapatikana katika gombo la Manabii Wadogo la Biblia, kwa jina la Kitabu cha Yoeli. Humo tunasoma alivyotangazwa siku tukufu ya Bwana na fumbo la Roho Mtakatifu kumiminwa juu ya kila mtu, ambalo Wakristo wanaamini Mwenyezi Mungu alilitimiza kwa namna ya ajabu katika Yesu Kristo kwenye Pentekoste [1].

Tangu kale anaheshimiwa kama mtakatifu.

Sikukuu yake kwa Wakatoliki na Waorthodoksi huwa tarehe 19 Oktoba[2][3] lakini awali pia tarehe 13 Julai.

Remove ads

Tazama pia

Tanbihi

Viungo vya nje

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads