Nestori

From Wikipedia, the free encyclopedia

Nestori
Remove ads

Nestori (kwa Kigiriki Νεστόριος, Nestorios; Germanicia, (leo nchini Uturuki) 386 hivi – al-Khargah, Misri, 450[1]) alikuwa mmonaki na mwanateolojia aliyefikia kuwa Patriarki wa Konstantinopoli (leo Istanbul) tangu tarehe 10 Aprili 428 hadi Agosti 431, ambapo kaisari Theodosius II alithibitisha uamuzi dhidi yake uliopitishwa na Mtaguso wa Efeso tarehe 22 Juni.

Thumb
Nestori kadiri ya Romeyn de Hooghe (1688)

Kwa kukataa jina lililozoeleka la Θεοτόκος, Theotokos, "Mama wa Mungu", kwa Bikira Maria, alisababisha mabishano makubwa na hatimaye mafarakano kuhusu fumbo la Yesu Kristo.

Hasa Sirili wa Aleksandria alimpinga vikali kwa kudai haamini umungu wa Yesu, ingawa mwenyewe alizidi kujitetea hadi kifo chake kwamba anashika imani sahihi.

Anaheshimiwa na Kanisa la Asiria kama mtakatifu. Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 25 Oktoba.

Remove ads

Tazama pia

Tanbihi

Vyanzo

Viungo vya nje

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads