Nothando Dube

Ufalme wa Swazi (1988–2019) From Wikipedia, the free encyclopedia

Remove ads

Nothando Dube (anajulikana kama Inkhosikati LaDube; 6 Februari 1988[1]– 8 Machi 2019) alikuwa mwanachama wa nyumba ya Dlamini kama Inkhosikati (Malkia mke) wa kumi na mbili na mke wa Mfalme Mswati III wa Eswatini.

Maisha Yake

Nothando Dube alikuwa Miss kijana wa Swaziland wa zamani.[2] Dube alisoma katika Shule ya Sekondari ya Mater Dorolosa.[3]Alikutana na Mswati III, mfalme wa Eswatini, mwaka 2004 katika sherehe ya kuzaliwa aliyoiandaa kwa ajili ya mmoja wa watoto wake. Aliamua kumuoa wakati wa ngoma ya manyasi aliyoshiriki pamoja na maelfu ya wanawake wengine wa Eswatini, iliyofanyika katika Kijiji cha Kifalme cha Ludzidzini.

Maisha kama mke

Mwaka 2005 aliolewa na Mswati III, akawa mke wake wa kumi na mbili, akiwa na umri wa miaka kumi na sita.[4] Alijifungua watoto watatu.[5][6] Mwaka 2010 alikuwa na uhusiano wa kimapenzi na Waziri wa Sheria Ndumiso Mamba, ambapo inasemekana aliwekwa chini ya kizuizi cha nyumbani.[7][8][9] Aliwasilisha malalamiko ya unyanyasaji na mateso kutoka kwa walinzi wa mfalme.[10] Baada ya mwaka mmoja chini ya kifungo cha nyumbani, alifukuzwa kutoka katika familia ya kifalme na kupigwa marufuku kuwaona watoto wake.[11]

Kifo

Alifariki mnamo tarehe 8 Machi 2019 katika hospitali nchini Afrika Kusini kutokana na saratani ya ngozi.[12][13] Kifo chake kilitangazwa rasmi na Gavana Lusendvo Fakudze kupitia Huduma ya Utangazaji na Habari ya Eswatini.[14] Alizikwa tarehe 11 Machi 2019.[15]

Remove ads

Marejeo

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads