Onesiforo

From Wikipedia, the free encyclopedia

Onesiforo
Remove ads

Onesiforo (jina la Kigiriki lenye maana ya "mleta faida") alikuwa mwanamume Mkristo wa karne ya 1 aliyetajwa na Mtume Paulo kwa shukrani katika Waraka wa pili kwa Timotheo 1:16-18.

Thumb
Mt. Onesiforo katika mchoro mdogo.

Sababu ni kwamba alimsaidia sana alipokuwa Efeso, halafu akamfuata hadi Roma mpaka akafaulu kumuona na kumfariji bila kuonea aibu minyororo yake.[1][2][3]

Kwa hiyo Paulo alimtakia huruma ya Mungu pamoja na familia yake.[4]

Inasemekana Onesiforo alipata kuwa askofu wa Kolofon (Asia Ndogo), halafu wa Korintho. Hatimaye alifia dini mjini Parium (karibu na Efeso)[5].

Tangu kale anaheshimiwa kama mtakatifu.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 6 Septemba[6][7] au kesho yake[8].

Remove ads

Tazama pia

Tanbihi

Viungo vya nje

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads