Onesimo
From Wikipedia, the free encyclopedia
Remove ads
Onesimo (kwa Kigiriki Ὀνήσιμος, Onēsimos, yaani "Wa kufaa"; labda alifia dini Roma, Italia, mwaka 68 hivi),[1] alikuwa mtumwa wa Filemoni, Mkristo tajiri wa Kolosai, leo nchini Uturuki.

Anaheshimiwa na madhehebu mbalimbali ya Ukristo kama mtakatifu.
Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 15[2] au 16 au 28 Februari, au tarehe 22 Novemba.
Remove ads
Katika Biblia
Jina "Onesimo" linatajwa katika Nyaraka mbili za Mtume Paulo: Waraka kwa Wakolosai 4:9[3] na Waraka kwa Filemoni ambao uliandikwa wote ili kumtetea.
Ni kwamba Onesimo alikuwa amemkimbia Filemoni na labda alimuibia pia. Lakini baadaye alikutana na Mtume Paulo (ama Roma ama Kaisarea)[4][5] akaongokea Ukristo. Paulo, aliyekuwa amekwisha kumuongoa Filemoni pia, aliamua kuwapatanisha kwa barua iliyomo sasa katika Agano Jipya.[6]).
Tazama pia
Tanbihi
Viungo vya nje
Wikiwand - on
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.
Remove ads