Oti
From Wikipedia, the free encyclopedia
Remove ads
Oti (kutoka Kiing. "oats") [1] ni mmea wa familia ya manyasi katika ngeli ya monokotiledoni. Mbegu au punje za oti ni nafaka ambayo ni chakula cha wanyama na pia cha watu katika nchi hasa za Ulaya na pia penginepo nje ya kanda ya tropiki. Tofauti na nafaka nyingi punje zake hazikai pamoja katika mshikano lakini ua lake linafanana zaidi na mpunga lakini mbegu ni tofauti kabisa.

Kihistoria ilikuwa chakula muhimu cha watu wa nchi za kaskazini kwa sababu inavumilia hali ya hewa baridi kiasi na mvua nyingi tofauti na ngano. Waroma waliona Wagermanik wa Kale walikula hasa oti; kwenye kisiwa cha Britania Waskoti hupenda oti lakini Waingereza hulisha nafaka hii kwa wanyama hasa farasi. Kupunguka kwa farasi kama wanyama wa kazi kwenye kilimo kumemaaanisha pia kurudi nyuma kwa kilimo cha oti.
Matumizi yake kwa binadamu ni katika uji, muesli, mkate na keki. Hutazamiwa kama chakula cha kujenga afya kutokana na wanga, vitamini na proteini ndaniy ake.
Remove ads
Marejeo
Wikiwand - on
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.
Remove ads