Ozoni
kiwanja cha kemikali From Wikipedia, the free encyclopedia
Remove ads
Ozoni (kutoka Kiingereza: ozone, pia trioxygen) ni molekuli yenye alama ya O3 inayofanywa na atomi tatu za oksijeni.

Tabia
Inaonekana kama gesi ya buluu yenye harufu kali. Inatokea katika matabaka ya juu ya angahewa ambako mnururisho wa urujuanimno unapasua molekuli za O2.
Inatokea pia katika mazingira ya mashine kama ya fotokopi zinazotumia volteji ya juu.
Si molekuli thabiti, hivyo inasambaratika tena baada ya muda.
Remove ads
Tabaka la ozoni
Ozoni hupatikana kwa viwango vidogo vya ppm 0.6 katika angahewa. Kiasi kikubwa kipo kwenye tabakastrato baina ya kilomita 10 hadi 50 juu ya uso wa ardhi. Tabaka hili lenye ozoni linafyonza asilimia kubwa ya mnururisho wa urujuanimno (93-99%) ulio hatari kwa viumbehai duniani.
Athari kwa viumbehai
Katika matabaka ya chini ya angahewa ozoni ni sumu kwa viumbehai ikitokea kwa viwango juu ya ppm 0.1. Kwa binadamu inaweza kukera pua na koo pamoja na kuleta kichefuchefu. Kuathiriwa kwa muda mrefu kunaweza kuleta kufura kwa mapafu[1].
Ppm 0.100 ni kiwango cha juu kinachoruhusiwa ndani ya karakana, viwanda au ofisi katika nchi kama Uingereza, Japani, Ufaransa, Uholanzi na Ujerumani.
Matumizi
Kutokana na nguvu yake ya kuoksidisha, ozoni hutumiwa kwa madhumuni mbalimbali:
Marejeo
Wikiwand - on
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.
Remove ads