Mgongo wa bahari ya Pasifiki-Antaktiki

From Wikipedia, the free encyclopedia

Mgongo wa bahari ya Pasifiki-Antaktiki
Remove ads

Mgongo wa bahari ya Pasifiki-Antaktiki ni mgongo kati wa bahari katika Bahari ya Pasifiki ya kusini na pia kwenye Bahari ya Kusini. Ni kama safu ya milima ya volkeno kwenye sakafu ya bahari.

Thumb
Mgongo wa bahari ya Pasifiki-Antaktiki inaonekana katika sehemu ya chini ya picha, juu yake mgongo wa bahari ya Pasifiki Mashariki na mgongo wa bahari ya Chile.

Unatenganisha Bamba la Pasifiki na Bamba la Antaktiki[1]. Mabamba hayo ya gandunia yanaachana kwa kasi ya milimita 54 na 76 kwa mwaka[2]. Kwenye mstari yanapoachana kuna ufa ambako magma moto kutoka koti ya Dunia inapanda juu ikiingia katika maji ya bahari ambako inapoa na kuganda. Kwa njia hiyo magma ikipoa inajenga safu ya milima.

Remove ads

Marejeo

Viungo vya Nje

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads