Mgongo wa bahari ya Pasifiki-Antaktiki
From Wikipedia, the free encyclopedia
Remove ads
Mgongo wa bahari ya Pasifiki-Antaktiki ni mgongo kati wa bahari katika Bahari ya Pasifiki ya kusini na pia kwenye Bahari ya Kusini. Ni kama safu ya milima ya volkeno kwenye sakafu ya bahari.

Unatenganisha Bamba la Pasifiki na Bamba la Antaktiki[1]. Mabamba hayo ya gandunia yanaachana kwa kasi ya milimita 54 na 76 kwa mwaka[2]. Kwenye mstari yanapoachana kuna ufa ambako magma moto kutoka koti ya Dunia inapanda juu ikiingia katika maji ya bahari ambako inapoa na kuganda. Kwa njia hiyo magma ikipoa inajenga safu ya milima.
Remove ads
Marejeo
Viungo vya Nje
Wikiwand - on
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.
Remove ads