Pamela Jelimo

Mkimbiaji wa mbio za kati wa Kenya From Wikipedia, the free encyclopedia

Pamela Jelimo
Remove ads

Pamela Jelimo (alizaliwa 5 Desemba 1989) ni mwanamichezo Mkenya aliyebobea katika mbio ya mita 800. Alishinda medali ya dhahabu kwenye Olimpiki ya mwaka wa 2008 mjini Beijing. Yeye ni mwanamke wa kwanza wa Kenya kushinda medali ya dhahabu ya Olimpiki na pia Mkenya wa kwanza kushinda Golden League Jackpot. Anashikilia rekodi ya dunia ya mita 800 ya wakiambiaji wachanga na rekodi ya Afrika ya wakimbiaji wazee wa umbali huo. Jelimo pia ni mmoja wa wanawake wachanga kuishindia Kenya medali ya dhahabu ya Olimpiki. Alishinda dhahabu hiyo ya mita 800 akiwa na umri wa miaka 18 tu.

Ukweli wa haraka Rekodi za medali, Women's Wanariadha ...
Remove ads

Maisha ya utotoni

Pamela Jelimo alizaliwa katika kijiji cha Kiptamok, wilaya ya Nandi, katika mkoa wa Bonde la Ufa. Mamake, Esther Cheptoo Keter, alikuwa mkimbiaji mzuri wa mita 200 na mita 400 lakini desturi za kikabila za Wanandi zilimaanisha kwamba kama binti ambaye ni kitinda mimba asingeweza kuolewa na ilimbidi awahudumie wazazi wake wenye umri wa makamo. Hata hivyo, alipewa ruhusa kuzaa watoto kwa wanaume tofauti, hivyo basi Jelimo alilelewa na mamake katika familia ya kaka watatu na dada wasita.[1] Jelimo alianza kukimbia mwaka wa 2003, akiwa na umri wa miaka 13, akiwa katika shule ya upili ya Koyo, divisheni Kaptumo, karibu na Kapsabet. [2] Alijifahamisha mwenyewe kama mwanamichezo aliyetimia kwa kushinda mashindao ya shule katika mita 100,mita 200 ,mita 400 , mita 800, mita 400 kutumia vikwazo na heptathlon. [3] Mwalimu wake wa michezo wa skuli ya upili, mwalimu Filipo N'Geno, alisema kwamba alikuwa akishindana na wavulana katika masafa mafupi kwani wasichana hawakumpa ushindani aliyohitaji.[1]

Familia yake ilikuwa maskini na ilijitahidi kulipa karo ya kumpeleka Jelimo katika shule ya upili - ndugu zake wawili wakubwa walikuwa tayari wameacha kusoma kwa hawakuweza kukidhi gharama. Yeye alikataa kuacha shule na alianza kuuza maziwa ya ng'ombe ya familia yake ili aweze kulipa karo.Alipitia miteremko kwa miguu iliaweze kuuza maziwa hayo katika soko la Chemase.[4] Mwalimu mkuu wa shule yao, Daniel Maru, alichangia fedha kwa ajili ya suti za maburuzo na viatu vya kukimbilia ili Jelimo aweze kuhudhuria kituo bora cha mbio cha masafa marefu nchini Kenya. Ilipotimia mwaka wa 2004, Jelimo alikuwa amefikia michuano ya mitaa ya mkoa katika mita 400.[2] Maru aliendelea na ukarimu wake. Alimruhusu Jelimo kuhitimu wakati bado alikuwa anadaiwa thamana ya mwaka mmoja ya karo. Hata hivyo, mamake alilazimishwa kuuza ng'ombe wake wa mwisho ndiposa Jelimo aweze kufanya mtihani wake.[1][3]

Manamo juni 2007, alimaliza wa tano katika mbio za mita 400 katika mashindano ya kitaifa ya Kenya kwa muda wa sekunde 55.82.[5] Aliendelea kujiboresha msimu wote. Alishinda medali ya dhahabu ya mita 400 katika mashindano ya Afrika ya wakimbiaji wachanga kwa kumaliza kwa muda wa sekunde 54.93 na kuweka rekodi ya kitaifa ya wakimbiaji wachanga ya Kenya katika mita 200 pamoja kwa sekunde 24.68. Jelimo alifurahishwa na mafanikio yake lakini kocha wake mpya, Zaid Kipkemboi Aziz, alipendekeza abadilishe na aanze kukimbia mita 800, kwa kusema kuwa atafanya bora katika mbio ya masafa marefu. Alianza kuifanyia kazi shurutisho la polisi la Kenya na alikuwa anafanya mazoezi na mwanariadha mkenya mwenzake Janeth Jepkosgei.

Jelimo alikimbia mbio yake ya kwanza ya mita 800 tarehe 19 Aprili 2008 katika majaribio ya Kenya ya michuano ya Afrika kwa muda wa dakika 2:01.02.[6] Lich ya masumbuko yake katika uanariadha wake, aliendelea kufanya kazi katika kituo cha Polisi cha Embu kama polisi na kupata shilingi 11000 kwa mwezi (kama euro 100).[7]

Remove ads

Kupanda Utukufu

Utukufu wake ulianza katika mashindano ya ubingwa wa Afrika mwaka wa 2008 Athletics akiwa na umri wa miaka 18.[8] Muda wake, 1:58.70, ulikuwa rekodi mpya wa wanariadha wachanga. Tarehe 25 Mei 2008 alishinda mbio za mita 800 katika Grand Prix laHengelo na kuweka rekodi mpya ya wanariadha wachanga kwa muda wa dakika 1:55.76. Rekodi ya zamani (1:57.18) iliwekwa na Yuan Wang wa China mwaka wa 1993.[9] Ilikuwa pia rekodi mpya ya Kenya ambayo awali ilikuwa inashikiliwa na Janeth Jepkosgei (1:56.04 mwaka wa 2007).[10] Tarehe 1 Juni 2008 alikimbia mbio ya kuvutia ya mita 800 huko Berlin na alishinda ISTAF Golden League kwa muda wa dakika 1:54.99, rekodi mpya ya Afrika. Rekodi ya awali ya Afrika (1:55.19) iliwekwa na Maria Mutola mwaka wa 1994.

Tarehe 18 Julai mwaka wa 2008, aliboresha rekodi hiyo kwa kiasi kidogo tu kwa muda wa dakika 1:54.97 mjini Paris. Huu pia ulikuwa ushindi wake wa nne mfululizo katika AF Golden League, ambapo yeye alikuwa mmoja kati ya wawili tu waliyobaki kama wagombeaji wa jackpot ,mwingine akiwa mrukaji Blanka Vlašić. [11] Tarehe 18 Agosti 2008 Jelimo alishinda dhahabu katika mita 800 katika Olimpiki ya Beijing. Muda wake ulikuwa 1:54.87, kwa mara nyingine tena rekodi. Akawa mwanamke wa kwanza wa Kenya kushinda medali ya dhahabu ya Olimpiki.[12]

Aliendeleza rekodi yake ya kutoshindwa kwa kushinda pambano la Weltklasse Golden League mjini Zürich tarehe 29 Agosti 2008 na kuboresha wakati wake wa kibinafsi hadi dakika 1:54.01.[13] Huu ulikuwa utendaji wa tatu wa kasi zaidi milele, nyuma ya Nadezhda Olizarenko na rekodi ya dunia ya Jarmila Kratochvílová. Katika mashindano ya ukumbusho wa Van Damme mjini Brussles, fainali ya AF Golden League, Jelimo alishinda mbio za mita 800 kwa muda wa 1:55.16.[14] Kama mwanariadha wa kipekee kushinda tukio moja (mbio ya mita 800) katika mikutano yote 6 ya Golden League, yeye alishinda shindano la jackpot la dola milioni 1. Mwanariadha yule mwingine aliyekuwa amebaki katika shindano hilo, Blanca Vlasic, alishindwa kushinda tukio la mwisho.[15] Yeye ni Mkenya wa kwanza kushinda Golden League jackpot.[16]

Alilikunja jamvi msimu wake wa kutoshindwa kwa kushinda mbio yake (mita 800) katika fainali ya IAAF World Athletics wa mwaka wa 2008. Baada ya tukio hilo alirejea Kenya kwa mara ya kwanza tangu majaribio ya Olimpiki na kukaribishwa na sikukuu nyingi. Tarehe 18 Septemba 2008 katika mji wa Kapsabet, njia - njia ya Pamela Jelimo (Pamela Jelimo Street)- ilitajwa kwa heshima yake.[17]

Jelimo aliorodheshwa katika jamii ya wanariadha wanawake bora mwaka huo na IAAF pamoja na Yelena Isinbayeva na Tirunesh Dibaba, lakini Isinbayeva alilishinda tuzo hilo. Hata hivyo, Jelimo alituzwa tuzo la Ufunuo wa mwaka wa IAAF (IAAF Revelation of the year Award) na tuzo la mwanamichezo mwanamke wa mwaka wa Kenya. [18][19]

Alikosa msimu wa ndani (indoor) wa 2009 kutokana na kunyooka kwa achilles wakati wa mazoezi.[20] Badala yake, alianza msimu wake mwezi wa Aprili katika pambano la Athletics Kenya huko Kakamega, na kukimbia mbio za mita 200 na 1,500 kwa ajili ya mazoezi.[21] Tarehe 23 Mei alikimbia mbio yake ya kwanza ya mita 800 ya mwaka wakati wa pambano la Kimataifa wa Mohammed wa VI mjini Rabat, Morocco, na kumaliza wa sita (muda wa 2:02.46) - hii ilikuwa mbio ya kwanza ya mita 800 ambayo hakushinda.[22] l Wiki mbili baadaye alimaliza wa mwaisho katika pambano la Prefontaine Classic huko Eugene, Oregon. [23] Kutokana na matokeo haya mabaya, alijinuiza kwa mazoezi kwa zaidi ya mwezi. Alifanikiwa kurejea mbioni kwa kushinda pambano la Heusden-Zolder tarehe 18 Julai kwa kukimbia chini ya dakika mbili (1:59.59).[24][25]

Alishindana katika mashindano ya dunia ya mwaka wa 2009 lakini hakumaliza nusu fainali yake.[26]

Remove ads

Maisha binafsi

Jelimo aliolewa na Petro Kiprotich Murrey, ambaye pia ni mkimbiaji wa mita 800, mwishoni mwa 2007. Hawakuwa na waya wa harusi kubwa; uwezo wao haukuwawezesha na badala yake walikuwa na sherehe ndogo. Ndoa haikufichuliwa kwa hadhara hadi Desemba 2008.[27].

Mafanikio

Ubora binafsi

Maelezo zaidi Tarehe, Tukio ...

Sahihi tangu 10 Oktoba 2008. Habari yote imetoka IAAF.

Rekodi ya mashindano

Maelezo zaidi mwaka, Michuano ...
Remove ads

Marejeo

Viungo vya nje

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads