Reichstag
From Wikipedia, the free encyclopedia
Remove ads
Reichstag(tamka: raikh-s-tag) ni neno la lugha ya Kijerumani linalotaja bunge la kihistoria la Ujerumani lakini pia jengo la bunge huko Berlin.

Reichstag kama bunge la watemi hadi 1806
Kiasili "Reichstag" ilikuwa mkutano wa watemi wote wa Dola Takatifu la Kiroma yaani Ujerumani [1] ulioitishwa na mfalme au kaisari. Mikutano ya aina ilijulikana tangu zamani za Kaisari Karolo Mkuu mnamo mwaka 800.
Baadaye Reichtag hadi mwaka 1806 ilikuwa mkutano wa wawakilishi wa watawala wadogo walioshauriana pamoja na kaisari au mwakilishi wake. Hapo ilikutana katika vikundi vitatu:
- kundi dogo la watemi wakuu wenye haki ya kupiga kura katika uchaguzi wa kaisari mpya; kwa jumla walikuwa kati ya 7 na 9.
- halmahauri ya watemi wa milki wenye wajumbe 100; watemi wakubwa zaidi walikuwa na kura zao lakini wale wadogo walishirikiana nafasi ya mjumbe 1.
- halmashauri ya miji ya milki yaani miji iliyojitegemea na haikuwa chini ya mtemi wowote.
Mwisho wa Dola Takatifu 1806 ulikuwa pia mwisho wa awamu hili la kwanza la Reichstag. Hali halisi halikuwa bunge kwa maana ya kisasa bali mkutano wa watemi au wawakilishi wao.

Remove ads
Bunge la Dola la Ujerumani 1871 - 1945
Bunge la kwanza lenye jina hili lilikuwa bunge la Shirikisho la Ujerumani ya Kaskazini tangu 1866 na 1970. Baada ya kuundwa kwa umoja wa Ujerumani kutokana na ushindi katika vita ya vita ya Ujerumani na Ufaransa ya 1870/71 bunge la Dola la Ujerumani lilipewa pia jina la "Reichstag". Likaendelea kwa jina hili kama bunge la milki ya Kaisari hadi 1918, kama bunge la Jamhuri ya Weimar hadi 1933 na mwishoni kama bunge la Dola la Tatu hadi 1945 mwaka ambako Dola la Ujerumani lilikwisha baada ya vita kuu ya pili ya dunia.

Remove ads
Jengo la mjini Berlin linaloitwa "Reichstag"
Wikiwand - on
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.
Remove ads