Teofilo wa Antiokia

From Wikipedia, the free encyclopedia

Teofilo wa Antiokia
Remove ads

Teofilo wa Antiokia (kwa Kigiriki Θεόφιλος ὁ Ἀντιοχεύς, Theofilos o Antiokheus, alifariki 183/185 BK) alikuwa askofu wa 7 wa Antiokia[1] baada ya Eros na kabla ya Masimo I[2][3].

Thumb
Mchoro mdogo unaomuonyesha.

Kutoka maandishi yake (Eusebi wa Kaisarea na Jeromu walitaja vitabu mbalimbali vya Teofilo vilivyokuwepo nyakati zao, ambavyo kati yake kimebaki kile Utetezi kwa Autolycus[4], rafiki yake msomi lakini Mpagani) tunajua kwamba alizaliwa na Wapagani katika eneo la kati ya mito Tigri na Eufrate, na kwamba aliingia Kanisa kwa kupendezwa na maadili ya Wakristo na kwa kusoma Biblia, hasa vitabu vya kinabii.[5]

Kutoka kwa mwanahistoria Eusebius wa Kaisarea tunajua juhudi zake za kutetea imani sahihi na kupinga uzushi, hasa ule wa Marcion[6][7], akichangia fasihi ya Kikristo, hoja za dini, ufafanuzi wa Biblia na utetezi wa dini kwa kutumia elimu yake pana.[8]

Maandishi yake ndiyo ya zamani kuliko yale yote tuliyonayo yanayotaja Utatu Mtakatifu.

Tangu kale anaheshimiwa na Wakatoliki na Waorthodoksi kama mtakatifu.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 13 Oktoba[9].

Remove ads

Tazama pia

Tanbihi

Viungo vya nje

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads