Toba

From Wikipedia, the free encyclopedia

Toba
Remove ads

Toba (kutoka neno la Kiarabu) ni msimamo wa mtu kujuta dhambi na kwa hiyo kutaka kurekebisha alichoharibu kwa njia hiyo.

Thumb
Shutuma ya Nabii Nathani dhidi ya Mfalme Daudi na toba ya huyo (Paris Psalter, folio 136v, karne ya 10).

Toba inaweza kujitokeza kwa matendo ya nje ambayo mtu anajipangia ili kubadilika na kufidia. Kati ya matendo hayo, kuna kusali, kusoma vitabu vya dini, kufunga, kujinyima n.k.

Wakristo wanafanya hivyo hasa wakati wa Kwaresima na Juma Kuu. Kwa namna tofauti, Majilio pia ni majira ya toba kwao.

Kwa Waislamu ni hasa mwezi mzima wa Ramadhani.

Remove ads

Katika Biblia

Kadiri ya Biblia, watu wote ni wakosefu na wanapaswa kufanya toba. Kwa sababu hiyo, bila toba hakuna wokovu.

Katika Ukristo

Ungamo la Augsburg linagawa toba pande mbili: "Mmoja ni majuto, yaani hofu inayochoma dhamiri kwa kutambua dhambi; wa pili ni imani ambayo inatokana na Injili au ondoleo, na kusadiki kwamba kwa ajili ya Kristo, dhambi zinasamehewa, na kufariji dhamiri na kuiokoa kutoka hofu."[1]

Katika baadhi ya madhehebu ya Ukristo, kama ya Wakatoliki na ya Waorthodoksi, toba inaweza kukamilishwa na sakramenti maalumu inayoitwa Kitubio au Upatanisho.

Remove ads

Tanbihi

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads