Utomvu

From Wikipedia, the free encyclopedia

Utomvu
Remove ads

Utomvu ni kiowevu kinachopitishwa katika seli za mimea. Unasafirisha maji na lishe ndani ya mmea[1].

Thumb
Utomvu wa mpira ukikusanywa mtini
Thumb
Kukusanya utomvu wa mnazi

Kutokana na aina mbili tofauti za seli za mimea, yaani zilemu na floemu, kuna aina mbili za utomvu wa zilemu na utomvu wa floemu[2].

Utomvu wa zilemu

Utomvu wa zilemu ni mmumunyo wa maji na homoni, madini na lishe nyingine, Mwendo wake ni kutoka mizizi kuelekea kwenye majani.

Utomvu wa floemu

Utomvu wa floemu ni mmumunyo wa maji na sukari, homoni na madini. Inashuka kutoka sehemu ambako kabohaidreti na sukari zinalishwa kwenda pale zinapohitajika, yaani kwenye sehemu ambako mmea unakua au sehemu ambako kabohaidreti zinatunzwa kama akiba.

Matumizi

Watu wametumia aina za utomvu, hasa ya floemu, tangu kale.

Marejeo

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads