Edomu

From Wikipedia, the free encyclopedia

Edomu
Remove ads
Remove ads

Edomu (kwa Kiebrania אֱדוֹם, Edom, ʼĔḏôm, yaani "nyekundu"[1]) au Idumea (kwa Kigiriki Ἰδουμαία, Idoumaía; kwa Kilatini Idūmaea) walikuwa taifa la Kisemiti lililoshi kusini kwa Bahari ya Chumvi katika eneo ambao leo limegawanyika kati ya Israeli na Yordan.

Thumb
Eneo husika lililokuwa mwaka 830 KK. Edomu inaonyeshwa kwa rangi ya njano.
Thumb
Ufalme wa Edomu (kwa rangi nyekundu) ulipofikia eneo kubwa zaidi, mwaka 600 KK hivi. Nyekundu iliyokolea inaonyesha mipaka ya kawaida zaidi ya Idumea.

Biblia inawataja mara nyingi kama washindani wa taifa la Waisraeli[2]ambao walikuwa na undugu kutokana na mababu wao kuwa watoto pacha wa Isaka, mwana wa Abrahamu.

Mataifa hayo mawili yaliendelea kushindana mpaka Edomu ilipomezwa na Israeli wakati wa Wamakabayo (karne ya 2 KK).

Baada ya hapo, Mwedomu Herode Mkuu alipata kuwa mfalme wa Israeli (37 KK - 4 KK) na kuacha ukoo ulioendelea kutawala kwa kwikwi chini ya himaya ya Dola la Roma kwa mwaka 100 hivi.

Remove ads

Tanbihi

Loading content...

Marejeo

Loading content...

Viungo vya nje

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads