Wastigmatini

From Wikipedia, the free encyclopedia

Wastigmatini
Remove ads

Wastigmatini (kutoka jina la Shirika la Madonda Matakatifu, ambayo kwa Kilatini yanaitwa Stigmata) ni shirika la kitawa la kikleri la Kanisa Katoliki. Jina rasmi ni Congregatio a Sacris Stigmatibus Domini Nostri Iesus Christi, kifupisho chake ni C.S.S.

Thumb
Mt. Gaspare Bertoni, mwanzilishi.

Historia

Wastigmatini walianzishwa na mtakatifu Gaspare Bertoni tarehe 4 Novemba 1816 huko Verona, Italia.

Katiba ya kwanza ilifuata kielelezo cha ile ya Wajesuiti iliyoandikwa na Ignas wa Loyola.

Shirika lilikua polepole: mwaka 1905 liliingia Marekani na mwaka 1910 Brazil.

Halafu China, Uthai, Ufilipino na nchi mbalimbali za Afrika (zikiwemo Afrika Kusini, Botswana, Ivory Coast, Tanzania) na Amerika (Kanada na Chile).

Mwaka 2002 lilifikia India.[1]

Remove ads

Takwimu

Mwaka 2012 walikuwa 422, wakiwemo mapadri 331, katika nyumba 92.

Utume

  • kulea vijana
  • kuhubiri mafungo na semina
  • kusaidia malezi ya kipadri

Tanbihi

Viungo vya nje

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads