Kitabu cha Zaburi
From Wikipedia, the free encyclopedia
Kitabu cha Zaburi ni kimojawapo kati ya vitabu vya Tanakh (yaani Biblia ya Kiebrania) na kwa hiyo pia vya Agano la Kale ambalo ni sehemu ya kwanza ya Biblia ya Kikristo.

Kama vitabu vingine vyote vya Biblia, hiki pia kinatakiwa kisomwe katika mfululizo wa historia ya wokovu ili kukielewa kadiri ya maendeleo ya ufunuo wa Mungu kwa binadamu.
Yaliyomo
Kina sura 150; kila sura ni zaburi moja. Zaburi ni aina ya sala iliyotungwa kama shairi au wimbo. Zaburi zinafundisha jinsi binadamu awezavyo kuzungumza na Mwenyezi Mungu.
Kwa hiyo kitabu cha Zaburi kinatumiwa na Wayahudi na Wakristo kama kitabu cha sala.
Mada za zaburi hasa ni sifa za Mungu, shukrani, maombolezo, huzuni na toba, furaha na imani, elimu ya kidini, na ombi la ushindi dhidi ya maadui wasiomcha Mungu.
Zaburi nyingi zimetungwa kama shairi la Kiebrania; mara nyingi fungu moja linarudia wazo la fungu lililopita, k.m. katika Zaburi 22, mistari 1-2:
- Mungu wangu, Mungu wangu, mbona umeniacha?
- Mbona uko mbali sana kunisaidia, mbali na maneno ya kilio changu?
- Ee Mungu wangu, nalia mchana lakini hujibu;
- napiga yowe usiku, lakini nafuu sipati.
Katika kitabu hicho zaburi kadhaa zimewekwa pamoja: kwa mfano, Zaburi za Wakorahi (baadhi zikiwa 42—49), za Asafu (73—83), za kumsifu Mungu aliye Mfalme au Mtawala wa wote (93—99) au Zaburi za kuhiji (120—134).
Baadaye Zaburi ziligawanywa katika vitabu vitano: 1—41; 42—72; 73—89; 90—106; 107—150. Kila kimojawapo kinamsifu Mungu katika mstari wake wa mwisho: 41:13; 72:19; 89:52; 106:48; na Zaburi yote ya 150. Inawezekana kuwa mgawanyo huo ulifanyika ili kuiga mgawanyo wa vitabu vitano vya kwanza vya Biblia, yaani Torati.
Baadhi ya Zaburi zinazojulikana sana ni:
Zaburi tatu fupifupi
Wikiwand - on
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.