Mchungaji

ukarasa wa maana wa Wikimedia From Wikipedia, the free encyclopedia

Mchungaji
Remove ads
Remove ads

Mchungaji ni mtu anayechunga mifugo, kama vile kondoo, lakini pia watu, hasa katika Ukristo, ambapo ni cheo maalumu katika madhehebu ya Uprotestanti.

Thumb
Mchungaji na kundi lake, mchoro wa mwaka 1905 hivi.
Thumb
Kristo akimuagiza Petro kadiri ya Raphael, 1515.
Thumb
Mchungaji wa Kimethodisti katika mavazi yake rasmi.

Kihistoria, uchungaji ulianza katika Mashariki ya Kati miaka 5,000 hivi iliyopita.

Katika Biblia kazi hiyo ilitumika sana kufafanua majukumu ya wafalme na viongozi wengine. Daudi alichukuliwa kama kielelezo.

Manabii walitabiri ujio wa mwana wa Daudi atakayechunga vizuri taifa la Israeli kwa niaba ya Mungu.

Yesu alijitambulisha kama mchungaji mwema aliye tayari kutoa uhai wake kwa ajili ya kondoo zake (Yoh 10:11).

Mwenyewe alimkabidhi Mtume Petro uchungaji wa kundi lake (Yoh 21:16).

Mfano huo unatumika pia kwa watu wengine (Mdo 20:17,28; 1Kor 9:7; Ef 4:11; 1Pet 5:12).

Katika ibada Maaskofu wa Kanisa Katoliki na wengineo wanatumia bakora kujitambulisha kama wachungaji.

Remove ads

Tazama pia

Tanbihi

Loading content...

Marejeo

Viungo vya nje

Loading content...
Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads