![cover image](https://wikiwandv2-19431.kxcdn.com/_next/image?url=https://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/3/36/Helsinki_July_2013-27a.jpg/640px-Helsinki_July_2013-27a.jpg&w=640&q=50)
Kanisa (jengo)
From Wikipedia, the free encyclopedia
Kuhusu jumuiya ya Wakristo angalia makala Kanisa
![Thumb image](http://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/3/36/Helsinki_July_2013-27a.jpg/640px-Helsinki_July_2013-27a.jpg)
Kanisa ni maabadi maalumu ya Wakristo. Hao, walipoanza kujenga mahali pa ibada, pakaja kuitwa kanisa kwa sababu ndani yake walikusanyika wao, Kanisa hai.
Hivyo hadi leo mara nyingi neno hilo linatumika kwa maana ya jengo. Mtume Paulo aliwahi kulinganisha umoja wa Wakristo na jengo aliloliita "nyumba ya Mungu", iliyojengwa juu ya msingi wa mitume na manabii, huku akimfananisha Yesu na jiwe kuu la msingi[1].