From Wikipedia, the free encyclopedia
Melchior Ndadaye (Machi 28, 1953 - Oktoba 21, 1993) alikuwa msomi wa sayansi na mwanasiasa. Yeye alikuwa wa kwanza kuchaguliwa kidemokrasia na wa kwanza wa kabila la Wahutu kuwa rais wa Burundi baada ya kushinda uchaguzi kuu wa kihistoria mwaka 1993.
Ingawa alijaribu kukomesha ukabila katika nchi hiyo, marekebisho yake yalishawishi askari katika jeshi lililotawaliwa na Watutsi, na aliuawa katikati ya mapinduzi ya kijeshi yaliyoshindwa mnamo Oktoba 1993, baada ya miezi mitatu tu ofisini.
Kuuliwa kwake kulizua idadi ya mauaji ya kikatili baina ya makabila ya Watutsi na Wahutu, na mwishowe yalizua Vita vya wenyewe kwa wenyewe vya Burundi vilivyodumu muongo mzima.
Mwaka 2020 mtangulizi wake Pierre Buyoya na wenzake wengi walihukumiwa kwenda jela maisha kwa kumuua[1]
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.
Every time you click a link to Wikipedia, Wiktionary or Wikiquote in your browser's search results, it will show the modern Wikiwand interface.
Wikiwand extension is a five stars, simple, with minimum permission required to keep your browsing private, safe and transparent.