Agabo
From Wikipedia, the free encyclopedia
Remove ads
Agabo (kwa Kigiriki Ἄγαβος, Agabos) alikuwa mmojawapo kati ya Wakristo wa kwanza kati ya Palestina na Siria.
Anatajwa mara mbili na kitabu cha Matendo ya Mitume kama nabii aliyeongozwa na Roho Mtakatifu[1].
Agabo anaheshimiwa kama mtakatifu na madhehebu mbalimbali ya Ukristo.
Sikukuu yake inaadhimishwa kila mwaka tarehe 13 Februari, 8 Machi au 8 Aprili[2][3].
Remove ads
Habari zake
Kadiri ya Mdo 11:27-28, alikuwa mmoja wa manabii waliofika Antiokia kutoka Yerusalemu na alitabiri njaa kali iliyotokea duniani kote wakati wa kaisari Klaudio.
Kadiri ya Mdo 21:10-12, miaka mingi baadaye (58 hivi BK), Agabo alikutana na Mtume Paulo huko Kaisarea Maritima akamtabiria atakavyokamatwa mapema na kuteswa na watu wa mataifa.
Kadiri ya mapokeo alikuwa mmojawapo kati ya wanafunzi 70/72 wa Yesu na alifia dini huko Antiokia, lakini hakuna hakika yoyote[4].
Remove ads
Tazama pia
Tanbihi
Marejeo
Wikiwand - on
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.
Remove ads