Ameriki
From Wikipedia, the free encyclopedia
Remove ads
Ameriki ni elementi ya kimetali yenye alama Am na namba atomia 95. Kwenye jedwali la elementi inahesabiwa ndani ya kundi la aktinidi. Ni metali laini yenye rangi ya kijivu-kifedha lakini inaoksidika haraka ikifunikwa na tabaka la oksidi kijivu-nyeusi.
Ameriki iligunduliwa mwaka 1944 katika maabara ya Chuo Kikuu cha Kalifornia pale Berkeley.
Ameriki ni elementi nururifu ambayo inatokea kiasili kwa viwango vidogo sana, inaundwa ndani ya madini ya urani kutokana mbunguo nururifu asilia ya urani. Nusumaisha ya isotopi zake ni hadi miaka 2,737, hivyo haiwezi kudumu muda mrefu kiasili. Inazalishwa katika tanuri nyuklia na maabara kwa kufyatulia nyutroni kwa plutoni.
Matumizi yake ni hasa katika vigunduzi moshi ambako inatumiwa kwa viwango vidogo ambavyo si hatari kwa afya.
Remove ads
Viungo vya Nje
- Americium at The Periodic Table of Videos (University of Nottingham)
- ATSDR – Public Health Statement: Americium
- World Nuclear Association – Smoke Detectors and Americium
![]() |
Makala hii kuhusu mambo ya kemia bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Ameriki kama historia yake au mahusiano yake na mada nyingine? Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |
Remove ads
Wikiwand - on
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.
Remove ads