Bakari (kundinyota)

From Wikipedia, the free encyclopedia

Bakari (kundinyota)
Remove ads

Bakari (Bootes kwa Kilatini na Kiingereza) [1] [2]. ni jina la kundinyota kwenye angakaskazi ya dunia yetu.

Thumb
Nyota za kundinyota Bakari (Bootes) katika sehemu yao ya angani

Mahali pake

Bakari ipo kati ya makundinyota ya Mashuke (pia Nadhifa, lat. Virgo) na Dubu Mkubwa (Great Bear). Njia Nyeupe inapita katika sehemu ya Bakari.

Jina

Bakari ilijulikana kwa jina hili kwa miaka mingi kati ya mabaharia Waswahili waliotumia nyota kutafuta njia baharini wakati wa usiku.[3]

Jina Bakari linatokana na ar. بقار baqqaar yaani "mchunga ng'ombe"[4]. Waarabu walipokea jina hili kutoka kwa elimu ya Wagiriki wa Kale kupitia Ptolemaio na kitabu chake cha Almagesti aliyetumia jina la Βοώτης boôtes[5]. Mitholojia ya Kigiriki iliona hapa picha ya Philomelos mwana wa mungu wa kilimo Demeter aliyebuni plau inayovutwa na maksai. Kwa hiyo Bakari ni yule anayeongoza maksai wanaovuta plau.

Lakini kuna mitholojia ya mbadala inayoona hapa mwindaji wa dubu. Kama jina lilikuwa kiasili Βοητης bo-e-tis maana yake ni "kuita kwa sauti kubwa" na inaweza kuunganishwa na hadithi ya mwindaji wa dubu (kundinyota jirani kwenye anga) anayeita mbwa wake.

Bakari-Bootes ni kati ya makundinyota yaliyotajwa tayari na Klaudio Ptolemaio katika karne ya 2 BK. Iko pia katika orodha ya makundinyota 88 ya Umoja wa kimataifa wa astronomia inapotajwa kama "Bootes"[6]

Remove ads

Nyota

Nyota angavu zaidi ni Simaki (α Alfa Bootis au Arcturus) inayojulikana pia kwa jina la kimataifa ya en:Arcturus yenye mwangaza unaoonekana wa −0.05 mag ikiwa umbali wa Dunia wa mwakanuru 36.7 (sawa na 11.26 parsek). Simaki ni nyota angavu zaidi ya nne angani.

Tanbihi

Marejeo

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads