Ben Pol

Mtanzania, mwimbaji na mtunzi wa nyimbo. From Wikipedia, the free encyclopedia

Remove ads

Bernard Michael Paul Mnyang’anga (anafahamika zaidi kwa jina lake la kisanii kama Ben Pol; amezaliwa 8 Septemba 1989) ni msanii wa muziki wa kizazi kipya na mwigizaji kutoka nchini Tanzania. Hasa anaimba muziki wa R&B.

Ukweli wa haraka Jina la kuzaliwa, Pia anajulikana kama ...

Ben Pol alianza kujulikana mnamo mwaka 2010 baada ya kutoa kibao cha "Nikikupata" ambacho kiliweza kumtambulisha katika ulimwengu wa Bongo Flava. Kwa asili Ben ni mtu wa Dodoma[1], tena anajisifu kama mtu kutoka kanda ya kati.

Remove ads

Nyimbo

Baadaye akaja kutamba zaidi na vibao kama vile

  • Samboira
  • Moyo Mashine
  • Jikubali
  • Phone
  • Nikikupata
  • Namba One Fan
  • TATU
  • Sophia


Upande wa filamu, amepata kucheza katika filamu ya Sunshine na baadhi tu ya filamu zilizokuwa chini ya MFDI Tanzania na kuongozwa na Karabani.[2]

Tuzo

Ameshinda tuzo za mziki Tanzania (KTMA) Kwa miaka mitatu mfululizo kudhibitisha ubora wake katika muziki wa R&B.

  • 2012
  • 2013
  • 2014

Ameshinda tuzo za www.mdundo.com

  • 2016

Tuzo za hipipo Uganda

  • 'Muzuki' wimbo bora wa Afrika Mashariki

Tazama pia

Marejeo

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads