Benwadi

From Wikipedia, the free encyclopedia

Benwadi
Remove ads

Benwadi wa Hildesheim (jina asili: Bernward; 96020 Novemba 1022) alikuwa askofu wa Hildesheim nchini Ujerumani kuanzia tarehe 15 Januari 993 hadi kifo chake[1] [2].

Thumb
Sanamu ya Mt. Benwadi huko Hildesheim.
Thumb
Kanisa la Mt Mikaeli lilijengwa na Benwadi.
Thumb
Milango ya Kanisa Kuu la Hildesheim iliagizwa na Benadi mnamo mwaka 1015.

Alilinda kundi lake dhidi ya maadui, aliendesha sinodi nyingi ili kurudisha nidhamu ya wakleri na alistawisha umonaki[3].

Benwadi aliagiza ujenzi wa kanisa kubwa la Mt. Mikaeli kwa mtindo wa Kiroma na pia kutengenezwa kwa milango ya shaba kwa kanisa kuu la Hildesheim; yote mawili yametambuliwa na UNESCO kama Urithi wa Dunia[4].

Papa Selestini III alimtangaza mtakatifu tarehe 19 Desemba 1192.

Sikukuu yake huadhimishwa na Wakatoliki na Waorthodoksi tarehe 20 Novemba[5].

Remove ads

Tazama pia

Tanbihi

Marejeo

Viungo vya nje

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads