Remove ads

Bibiarusi (pia biarusi, biharusi, bibiharusi) ni jina ambalo mwanamke huitwa siku chache kabla na baada ya kufunga ndoa.

Thumb
Arusi ya Yosefu na Maria.
Thumb
Msichana na beberu mwenye pembe moja tu, aliyetazamwa kumaanisha ubikira wake.
Thumb
Bango dhidi ya ukeketaji na ndoa ya kulazimishwa.

Katika Ukristo

Katika Ukristo (k. mf. Ufu 22:17) ni jina la Kanisa katika uhusiano wake na Yesu Kristo ulivyoelezwa na Mtume Paulo hasa katika Waraka kwa Waefeso (5:22-33). Mfano huo uliendelezwa na Mababu wa Kanisa, kama Ireneo wa Lyon na wengineo.

Hapo Yesu anatazamwa kama Adamu mpya, mkuu wa binadamu wote: kama vile kutoka ubavu wake akiwa usingizini aliumbwa Eva, vivyo hivyo kutoka ubavu wa Kristo uliotobolewa akiwa maiti msalabani (Yoh 19:31-35) lilitolewa Kanisa, bibiarusi wake, likiwakilishwa na maji na damu vilivyodokeza sakramenti za ubatizo na ekaristi zinazoliunda.

Remove ads
Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads