Bibiarusi (pia biarusi, biharusi, bibiharusi) ni jina ambalo mwanamke huitwa siku chache kabla na baada ya kufunga ndoa.



Katika Ukristo
Katika Ukristo (k. mf. Ufu 22:17) ni jina la Kanisa katika uhusiano wake na Yesu Kristo ulivyoelezwa na Mtume Paulo hasa katika Waraka kwa Waefeso (5:22-33). Mfano huo uliendelezwa na Mababu wa Kanisa, kama Ireneo wa Lyon na wengineo.
Hapo Yesu anatazamwa kama Adamu mpya, mkuu wa binadamu wote: kama vile kutoka ubavu wake akiwa usingizini aliumbwa Eva, vivyo hivyo kutoka ubavu wa Kristo uliotobolewa akiwa maiti msalabani (Yoh 19:31-35) lilitolewa Kanisa, bibiarusi wake, likiwakilishwa na maji na damu vilivyodokeza sakramenti za ubatizo na ekaristi zinazoliunda.
| Makala bado ni mbegu. Unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuongezea habari. |
Remove ads
Wikiwand - on
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.
Remove ads