Adamu mpya

From Wikipedia, the free encyclopedia

Adamu mpya
Remove ads

Adamu mpya, Adamu wa pili au Adamu wa mwisho (1Kor 15:45) ni kati ya majina ya Yesu katika Agano Jipya.[1][2][3]

Thumb
Utukufu wa mtoto Kristo mbele ya Mungu Baba na Roho Mtakatifu. Sehemu ya mchoro wa Daniel Gran Vienna, Austria. Adamu na Eva wamechorwa chini wamefungwa minyororo.
Thumb
Yesu akiwatoa Adamu na Eva nje ya makaburi yao siku ya kiyama, Istanbul, Uturuki.

Humo mara mbili Mtume Paulo anafananisha Yesu na Adamu.

Katika 1Kor 15:22 anasema, "kama vile katika Adamu wote wanakufa, vivyo hivyo katika Kristo wote watafanywa hai" na katika mstari wa 45 unamuita Yesu "Adamu wa mwisho".

Halafu katika Rom 5:12–21 anasema, "kama vile kwa kosa la mtu mmoja wengi wamefanywa wakosefu, vivyo hivyo kwa utiifu wa mmoja wengi watafanywa waadilifu" (Rom 5:19).

Remove ads

Katika teolojia

Kutokana na Yesu kuitwa Adamu mpya, Bikira Maria alifananishwa na Eva kuanzia karne ya 2 (Irenei), kwa jinsi alivyoshirikiana naye kama Eva mpya.

Katika Kurani

Quran pia inafananisha Yesu na Adamu kwa jinsi walioumbwa[4].

Tazama pia

Tanbihi

Marejeo

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads