Bwiru

From Wikipedia, the free encyclopedia

Bwiru
Remove ads

Bwiru ni ndege wadogo wa jenasi Platysteira katika familia Platysteiridae wanaotokea Afrika chini ya Sahara. Zamani waliainishwa katika familia Muscicapidae. Ndege hawa wana ngozi tupu nyekundu au buluu juu ya au pande zote za macho. Kwa kawaida ni weusi juu na weupe chini na wana mlia mweusi kidarini. Mara nyingi dume ana koo jeupe na jike koo jeusi au kahawia. Hula wadudu na hulijenga tago lao kwa uvumwani na utando wa buibui kwa umbo wa kikombe katika mti au kichaka. Jike huyataga mayai 2-4.

Maelezo zaidi Uainishaji wa kisayansi ...
Remove ads

Spishi

Remove ads

Picha

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads