Kwanza (mto)

From Wikipedia, the free encyclopedia

Kwanza (mto)
Remove ads

Kwanza (kwa Kireno: Cuanza, pia Coanza, Quanza au Kuanzani) ni mto katika Angola. Chanzo chake ni katika Nyanda za Juu za Bie ambako mito mingi mikubwa inaanza.

Ukweli wa haraka

Jina la mto limekuwa pia jina la mikoa miwili ya Cuanza Norte (kaskazini kwa mto) na Cuanza Sul (kusini kwa mto).

Matawimto muhimu ni Kuiva, Luando na Lucala.

Thumb
Remove ads

Mwendo wa mto

Mwanzoni mto unaelekea kaskazini halafu kaskazini-magharibi ikiwa mpaka kati ya mikoa ya Bie na Malange, baadaye kati ya mikoa ya Cuanza Sul na Malange, halafu kati ya mikoa ya Cuanza Sul na Bengo. Ikielekea magharibi inapita mkoa wa Cuanza Norte hadi kufikia Atlantiki kusini kwa Luanda, mji mkuu wa Angola.

Umuhimu wa kiuchumi

Kwanza inatumika na meli kwa mwendo wa takriban km 250 kuanzia mdomo wake kungia barani. Kwa sababu hiyo ilikuwa pia njia ya Wareno ya kupeleleza Angola walipofika na kujenga utawala wao.

Kwanza inatumika kwa kutengeneza umeme kwa njia ya lambo la Capanda mkoani Malanje lililoanza kufanya kazi mwaka 2004.

Bado inatumika kama njia ya kusafirisha mizigo, pia maji yake humwagilia mashamba.

Makala hii kuhusu maeneo ya Angola bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Kwanza (mto) kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.
Remove ads
Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads