Dudumizi

Ndege wakubwa kiasi wa jenasi Centropus, familia Cuculidae From Wikipedia, the free encyclopedia

Dudumizi
Remove ads

Dudumizi ni ndege wakubwa kadiri wa jenasi Centropus, jenasi pekee ya nusufamilia Centropodinae katika familia Cuculidae. Wana macho mekundu na mkia mrefu, na ukucha wa kidole kikabilicho nyuma ni mrefu sana. Jina “Centropus” linatoka maneno ya Kiyunani: κεντρον = mwiba na πους = mguu. Spishi nyingi zina mabawa kahawianyekundu na kichwa cheusi. Dudumizi hula wadudu, mijusi, nyoka na wanyama wadogo, na mayai, makinda, matunda na mizoga pia. Tago lao hujengwa katika uoto mzito na mara nyingi juu yake imefungwa. Jike hutaga mayai 2-5, lakini dume, ambaye ni mdogo zaidi, huatamia na hutunza makinda.

Maelezo zaidi Uainishaji wa kisayansi, Ngazi za chini ...
Remove ads

Spishi za Afrika

Remove ads

Spishi za Asia

Remove ads

Spishi ya kabla ya historia

Picha

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads