Eleazari mfiadini

From Wikipedia, the free encyclopedia

Eleazari mfiadini
Remove ads

Eleazari mfiadini (karne ya 3 KK - karne ya 2 KK) alikuwa mzee Myahudi aliyekubali kuuawa katika dhuluma ya mfalme Antioko Epifane kuliko kula nyama haramu au kudanganya kama kwamba ameila.

Thumb
Kifodini cha Eleazari mwandishi kadiri ya Gustave Doré, 1866.

Akipendelea hivyo kifo kitukufu kuliko maisha ya aibu, alitangulia kishujaa wengine kwenda mahali pa mateso na kuacha mfano mzuri ajabu wa uadilifu[1][2].

Habari zake zinasimuliwa katika kitabu cha pili cha Wamakabayo, sura ya 6.

Tangu kale anaheshimiwa na Wakatoliki, Waorthodoksi na Waorthodoksi wa Mashariki kama mtakatifu mfiadini.

Sikukuu yake inaadhimishwa hasa tarehe 1 Agosti[3].

Remove ads

Tazama pia

Tanbihi

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads