Helier Mtakatifu

From Wikipedia, the free encyclopedia

Helier Mtakatifu
Remove ads

Helier Mtakatifu (alifariki 555) alikuwa mkaapweke anaheshimika kama mmisionari wa kisiwa cha Jersey, karibu na Ufaransa[1].

Thumb
Mt. Helier katika kioo cha rangi, basilika la Tongeren, Ubelgiji.

Tangu kale anaheshimiwa kama mtakatifu mfiadini.

Sikukuu yake huadhimishwa na Wakatoliki, Waorthodoksi na Waanglikana tarehe 16 Julai[2].

Maisha

Thumb
Kikanisa kilichojengwa katika Karne za Kati juu ya pango alimoishi ("St. Helier's Bed"). Ndilo lengo la hija ya kila mwaka.

Mtoto wa wazazi tajiri wa Tongeren (leo nchini Ubelgiji). Ingawa Wapagani walikubali mtoto alelewe Kikristo, ila walipomuua Kunibert, mlezi wake, Helier alitoroka nyumbani.

Hatimaye alifikia Cotentin alipojiunga na monasteri ya Marcouf huko Nantus (Nanteuil, sasa St.-Marcouf-de-l’Isle, Manche).

Ni Marcouf aliyempeleka pamoja na padri Romard kuinjilisha Jersey ambapo hatimaye aliuawa na maharamia kwa kukatwa kichwa[3].

Remove ads

Tazama pia

Tanbihi

Vyanzo

Viungo vya nje

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads