Felisi wa Nicosia

From Wikipedia, the free encyclopedia

Felisi wa Nicosia
Remove ads

Felisi wa Nicosia, O.F.M.Cap. (jina la awali Filippo Giacomo Amoroso) alikuwa bradha wa shirika la Ndugu Wadogo Wakapuchini kutoka Sicilia, leo nchini Italia (5 Novemba 171531 Mei 1787).

Thumb
Mt. Felisi akibeba mkoba wa kuombea msaada kwa ajili ya konventi.

Baada ya kukataliwa miaka 10, alipopokewa utawani alitoa kwa unyofu na usafi wa moyo huduma duni alizoagizwa [1].

Ni maarufu hasa kwa utiifu wake wa ajabu, uliothibitishwa na kiongozi aliyejichukulia jukumu la kumjaribu na kumdhalilisha kwa kila namna.[2]

Papa Leo XIII alimtangaza mwenye heri tarehe 12 Februari 1888, halafu Papa Benedikto XVI alimtangaza mtakatifu tarehe 23 Oktoba 2005.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe aliyoaga dunia[3].

Remove ads

Tazama pia

Tanbihi

Marejeo ya Kiswahili

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads