Filipo wa Yesu

From Wikipedia, the free encyclopedia

Filipo wa Yesu
Remove ads

Filipo wa Yesu (1572 - 1597) alikuwa bradha wa shirika la Ndugu Wadogo Pekupeku kutoka Meksiko na mmisionari aliyefia dini Japani [1].

Thumb
Sanamu ya Mt. Felipe wa Yesu kwenye Museo del Virreinato, Tepotzotlán, Meksiko.

Dhuluma dhidi ya Wakatoliki zilipozidi, yeye na wenzake 25 (mapadri na watawa 8 na walei 17[2]) walikamatwa, walitukanwa na kuteswa vikali, na hatimaye wakasulubiwa huko Nagasaki tarehe 5 Februari mwaka 1597, huku wakifurahia neema ya kuuawa namna ileile ya Yesu [3].

Anaheshimiwa na Kanisa Katoliki kama mtakatifu mfiadini.

Sikukuu yake na ya wafiadini wenzake huadhimishwa kila mwaka tarehe 6 Februari[4].

Remove ads

Tazama pia

Tanbihi

Marejeo ya Kiswahili

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads