Fransisko wa Fatima

From Wikipedia, the free encyclopedia

Fransisko wa Fatima
Remove ads

Fransisko Marto wa Fatima (11 Juni 1908 - 4 Aprili 1919), ni jina la mmojawapo kati ya watoto watatu waliotokewa na malaika wa amani (1916), halafu na Bikira Maria (1917) kwao Fatima, Ureno, pamoja na binamu yake Lusia Santos na dada yake Yasinta Marto.

Thumb
Picha halisi ya Lusia Santos (kushoto) na binamu zake Fransisco na Yasinta Marto, mwaka 1917.
Thumb
Mahali pa Fatima nchini Ureno.
Thumb
Sanamu iliyotiwa taji ya Bikira Maria ya Fatima katika kikanisa kilichopo mahali pa njozi.

Njozi hizo zilithibitishwa na Kanisa Katoliki kuwa za kuaminika[1], hata ikaanzishwa kumbukumbu ya Bikira Maria wa Fatima katika liturujia kila tarehe ya njozi ya kwanza, 13 Mei.

Fransisko, katika miezi iliyofuata na ugonjwa uliommaliza, aling’aa kwa maadili, kwa kuvumilia tabu, kwa imani na kwa kudumu katika sala[2].

Pamoja na dada yake mdogo Yasinta, alitangazwa na Papa Yohane Paulo II kuwa mwenye heri tarehe 13 Mei 2000, halafu na Papa Fransisko kuwa mtakatifu tarehe 13 Mei 2017, miaka 100 kamili tangu tukio la kwanza.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe ya kifo chake[3].

Remove ads

Tazama pia

Tanbihi

Marejeo ya Kiswahili

Marejeo ya lugha nyingine

Viungo vya nje

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads