Fransisko wa Fatima
From Wikipedia, the free encyclopedia
Remove ads
Fransisko Marto wa Fatima (11 Juni 1908 - 4 Aprili 1919), ni jina la mmojawapo kati ya watoto watatu waliotokewa na malaika wa amani (1916), halafu na Bikira Maria (1917) kwao Fatima, Ureno, pamoja na binamu yake Lusia Santos na dada yake Yasinta Marto.


Njozi hizo zilithibitishwa na Kanisa Katoliki kuwa za kuaminika[1], hata ikaanzishwa kumbukumbu ya Bikira Maria wa Fatima katika liturujia kila tarehe ya njozi ya kwanza, 13 Mei.
Fransisko, katika miezi iliyofuata na ugonjwa uliommaliza, aling’aa kwa maadili, kwa kuvumilia tabu, kwa imani na kwa kudumu katika sala[2].
Pamoja na dada yake mdogo Yasinta, alitangazwa na Papa Yohane Paulo II kuwa mwenye heri tarehe 13 Mei 2000, halafu na Papa Fransisko kuwa mtakatifu tarehe 13 Mei 2017, miaka 100 kamili tangu tukio la kwanza.
Remove ads
Tazama pia
Tanbihi
Marejeo ya Kiswahili
Marejeo ya lugha nyingine
Viungo vya nje
Wikiwand - on
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.
Remove ads