Fransisko wa Fabriano

From Wikipedia, the free encyclopedia

Fransisko wa Fabriano
Remove ads

Fransisko Venimbeni wa Fabriano (2 Septemba 1251 - 22 Aprili 1322) alikuwa padri wa Kanisa Katoliki na mtawa wa shirika la Ndugu Wadogo kutoka Fabriano (Marche, Italia).

Thumb
Jumba la Meya wa Fabriano, lililojengwa wakati wa utoto wa Fransisko Venimbeni.

Mapema alianza kuheshimiwa kama mwenye heri. Hatimaye Papa Pius VI alithibitisha uhalali wa heshima hiyo tarehe 1 Aprili 1775.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe ya kifo chake[1].

Remove ads

Maisha

Kisha kumaliza masomo yake ya sayansi za jamii na falsafa, alijiunga na Wafransisko mwaka 1267, akajikita katika masomo ya teolojia, uandishi na utume katika mji wake asili na maeneo ya kandokando.

Alikuwa wa kwanza kuipatia konventi ya shirika lake maktaba kubwa.

Maandishi

Maandishi yake ("Chronica Marchiæ et Fabriani", "De veritate et excellentiâ Indulgentiæ S. Mariæ de Portiuncula", "Opusculum de serie et gestis Ministrorum Generalium", "Ars Prædicantium", mbali na "Hotuba" na vitabu vingine) yamepotea karibu yote.

Tanbihi

Viungo vya nje

Loading content...
Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads