George Saitoti
From Wikipedia, the free encyclopedia
Remove ads
Prof George Kinuthia Saitoti (3 Agosti 1945[1] - 10 Juni 2012) alikuwa mwanahisabati na mwanasiasa wa Kenya. Aliwahi kuwa Makamu wa Rais na alifariki akiwa Waziri wa Usalama wa Ndani.

Wasifu na elimu
Saitoti anayedaiwa kuwa Mmasai, lakini wapinzani na wadadisi wake wanasema alikuwa Mkikuyu. [2] kijugumu, Human Rights Watch walimshutumu kuchochea ghasia za kikabila katika Mkoa wa Rift Valley wakati wa uchaguzi mkuu wa Kenya wa mwaka 1992, vurugu ambayo ilielekezwa dhidi ya jamii ya Wakikuyu.[3]
Alisomea Shule ya Upili ya Mang'u na alipata elimu yake ya shahada ya kwanza huko Marekani katika Chuo Kikuu cha Brandeis baada ya kulipiwa na Wien. Saitoti alipata PhD katika Hisabati kutoka Chuo Kikuu cha Warwick mwaka 1972 katika nyanja ya algebraic topology.
Tarehe 30 Agosti 2002, Saitoti aliondolewa kama Makamu wa Rais na Rais Daniel Arap Moi kwa utovu wa nidhamu; Saitoti aliondolewa katika nafasi yake kama Makamu Mwenyekiti wa Kenya African National Union (KANU) [2]. Katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2002, alishinda kiti cha Kajiado North kwa chama cha NARC.
Remove ads
Kashfa ya Goldenberg na baadaye
Siku ya 13 Februari 2006 kujiuzulu kwa Saitoti kama Waziri wa Elimu ulitangazwa na Rais Mwai Kibaki katika televisheni, baada ya madai kwamba alikuwa amehusika katika kashfa ya Goldenberg. [4] Mahakama kuu ya Kenya iliamuru tarehe 31 Julai 2006 kuwa Saitoti haipaswi kushtakiwa juu ya kashfa ya Goldenberg.[5] Tarehe 15 Novemba 2006 alirudishwa kazini kama Waziri wa Elimu na rais Kibaki.[6]
Katika Bunge lililotangazwa na Kibaki 8 Januari 2008, kufuatia utata wa Uchaguzi wa 2007, Saitoti alikuwa Waziri wa Usimamizi wa Majimbo na Usalama wa Ndani katika Ofisi ya Rais.[7] Baada ya ugawaji madaraka kufikiwa kati ya Kibaki na Raila Odinga, wote ambao alidai ushindi katika uchaguzi wa 2007, Saitoti alihifadhi kazi yake katika Bunge la muungano lililotajwa tarehe 13 Aprili 2008.[8]
Saitoti alitangaza nia yake ya kuwania kiti cha Rais wa Kenya mwaka 2012.
Remove ads
Nafasi
- Waziri wa Fedha (1983 - 1988)
- Makamu wa Rais (Mei 1989 - Desemba 1997)
- Waziri wa Mipango na Maendeleo ya Taifa (Desemba 1997 - Aprili 1999)
- Makamu wa Rais (Aprili 1999 - 30 Agosti 2002)
- Waziri wa Elimu (Januari 2003 - Novemba 2005)
- Waziri wa Elimu (7 Desemba 2005 - 13 Februari 2006)
- Waziri wa Elimu (Novemba 2006 - Januari 2008)
- Waziri wa Usimamizi wa Majimbo na Usalama wa Ndani (Januari 2008 - hadi Juni 10 2012 alipofariki kutokana na ajali ya ndege ya helikopta ya Polisi walipokuwa wanasafiri kuchangisha ujenzi wa kanisa katika eneobunge(jimbo) la Naibu Waziri wake Josua Ojode, ambaye pia alifariki katika ajali hii, pamoja na wasaidizi wao wawili na marubani wawili wa ndege hiyo.
Marejeo
Viungo vya nje
Wikiwand - on
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.
Remove ads